25
Bildadi Anasema: Mwanadamu Awezaje Kuwa Mwadilifu Mbele Za Mungu? 
 1 Ndipo Bildadi Mshuhi akajibu: 
 2 “Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu; 
yeye huthibitisha amani katika mbingu juu. 
 3 Je, majeshi yake yaweza kuhesabika? 
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake? 
 4 Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu? 
Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi? 
 5 Ikiwa hata mwezi sio mwangavu 
nazo nyota si safi machoni pake, 
 6 sembuse mtu ambaye ni funza: 
mwanadamu ambaye ni buu tu!”